Mkutano wa 12 Bunge kuanza kesho

0
2241

Mkutano wa Kumi na Mbili wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unatarajiwa kuanza Septemba Nne na kumalizika Septemba 14 mwaka huu kwa kufanya shughuli mbalimbali.

Shughuli hizo ni pamoja na kupitisha kwa hatua zilizobaki miswada Mitano ya sheria ambayo ilisomwa kwa mara ya kwanza katika mkutano wa Kumi na Moja.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jijini Dodoma na Kitengo cha Habari, Elimu kwa Umma na Mawasiliano cha Ofisi ya Bunge imesema kuwa shughuli nyingine itakayofanyika ni kula kiapo cha uaminifu kwa Mhandisi Christopher Chizza ambaye ni Mbunge wa jimbo la Buyungu mkoani Kigoma aliyechaguliwa katika uchaguzi mdogo wa ubunge uliofanyika Agosti 12 mwaka 2018.

Maswali 125 ya kawaida yataulizwa na mengine 16 ya papo kwa papo yataulizwa kwa Waziri Mkuu wakati wa mkutano huo wa 12 wa Bunge.