Mitihani kidato cha nne yaanza nchini

0
1781

Mitihani ya kidato cha nne na mitihani ya maarifa –QT imeanza nchini kote huku hali ya ulinzi na ukimya vikiwa vimetawala.

Mwandishi wa TBC amepita katika shule mbalimbali za sekondari jijini Dar Es Salaam na kushuhudia hali ya ulinzi ikiwa imeimarishwa.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania –NECTA, Dkt. Charles Msonde ameiambia TBC kuwa mitihani hiyo imeanza vizuri kwa kuwa mitihani ilifika kwa wakati katika maeneo yote kunakofanyika mitihani.