Miili ya watu 172 yatambuliwa Ukara

0
2163

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema miili ya watu 172 waliokufa maji baada ya kivuko cha MV Nyerere kuzama Septemba 20 mwaka huu imetambuliwa hadi majira ya saa 11 jioni ya leo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika kisiwa cha Ukara mkoani Mwanza Waziri Kamwelwe amesema miili ya watu 112 imekwishachukuliwa na ndugu zao na miili ya watu 37 bado haijatambuliwa.Idadi ya miili ya watu iliyoopolewa imefikia 209.

Amesema wadau mbalimbali wameendelea kujitokeza kuchangia fedha kusaidia shughuli za uokoaji, misaada na rambirambi kwa waliofiwa ikiwemo Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo iliyotoa shilingi Milioni 150, Jumuiya ya Shia Dar Es Salaam imetoa shilingi Milioni 10 na zaidi ya katoni elfu tatu za maji, Wakala wa Ufundi na Umeme – TEMESA umeahidi kutoa mafuta kwa ajili ya kusafirisha miili ya marehemu na kutoa vifaa vitakavyotumika kunyanyua kivuko hicho kilichozama.