Miili ya waliouawa Songwe yapatikana

0
2459

Miili ya watu watatu wanaodaiwa kuuawa imepatikana kando ya Mto Mlowo wilaya ya Mbozi mkoani Songwe.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Songwe, – Mathias Nyange amewataja watu hao waliouawa kuwa ni Lucas Umri na mke wake Bahati Mohamed pamoja na mdogo wake maarufu kwa jina la mama Bina, ambapo inadaiwa watu waliotekeleza mauaji hayo walitumia vitu vizito.

Kamanda Nyange amesema kuwa ndugu mmoja wa marehemu hao ambaye walikuwa wanaishi naye ametoweka baada ya kutokea kwa mauaji hayo na kwamba jeshi la polisi mkoani Songwe linaendelea kumtafuta pamoja na kuendelea na upepelezi zaidi kuhusu tukio hilo.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Songwe, – Brigedia Jenerali Nichodemus Mwangela amewaomba wakazi wa mkoa huo kuwa watulivu wakati jeshi la polisi mkoani humo likiendelea na uchuguzi wake.

Pia ametoa wito kwa mtu yeyote mwenye taarifa kuhusu mauaji hayo atoe taarifa hizo kwenye vyombo vya sheria.