Miaka 55 ya Mapinduzi yaadhimishwa Pemba

0
1055

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dokta Ali Mohamed Shein amewataka watumishi wa umma kuongeza kasi ya kutekelaza wajibu wao kwa ufanisi ili kutatua na changamoto zinazowakabili wananchi.

Dokta Shein amesema hayo Kisiwani Pemba katika Kilele cha Maaadhimisho ya Miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo amesema watumishi wanatakiwa kufanya kazi kwa vitendo na kuongeza kiwango cha uzalendo katika kutekeleza majukumu yao.

Pia akaelezea mafanikio ya sekta mbalimbali katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ikiwemo sekta ya uchumi.

Kilele cha Maadhimisho ya Miaka hamsini na tano ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yamepambwa na vikundi mbalimbali vya ngoma pamoja na maonesho maalum ya Jeshi la Wananchi na Jeshi la Polisi.

Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanyika mwaka 1964 yaliyokuwa na lengo la kumkomboa mwananchi kutoka kwenye utawala wa kikoloni.