Mgodi wa kokoto wa Tan- Turk wafungwa

0
1949

Naibu Waziri wa Madini Doto Biteko ameufunga mgodi wa kokoto wa Tan- Turk ulipo katika kijiji cha Mindutulieni wilayani Bagamoyo  mkoani Pwani  hadi  hapo mmiliki wa mgodi huo atakapowalipa fidia wananchi wanaozunguka mgodi huo.

Naibu Waziri Biteko ametangaza kuufunga mgodi huo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wakazi wa kijiji  hicho ambao wamedai kuwa shughuli za ulipuaji wa baruti katika miamba  zinazofanywa katika mgodi zimekua zikisababisha mawe makubwa kuruka na kuangukia  katika makazi ya watu,  jambo linalohatarisha maisha yao.

Akizungumza mara baada ya kukagua mgodi huo wa kokoto wa Tan- Turk , Naibu Waziri Biteko amemuagiza mmiliki wake  kutofanya shughuli zozote hadi hapo atakapozilipa fidia  kaya zaidi ya Thelathini zilizopo katika eneo la mgodi.

Akiwa katika mgodi huo, Naibu Waziri Biteko pia ameelezea kutoridhishwa  na utunzaji wa kumbukumbu za  kiwango cha  kokoto kinachouzwa ndani ya mgodi huo, hali inayosababisha serikali kukosa mapato.