Mazishi ya waliokufa maji yanafanyika Ukara

0
2380

Mazishi ya Kitaifa ya watu waliokufa maji katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere yanaendelea hivi sasa katika kisiwa cha Ukara.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ndiye anayeongoza mazishi hayo ambayo pia yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali.

Akizungumza na TBC mapema hii leo, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema kuwa kazi ya kuokoa miili ya watu waliokufa maji katika ajali hiyo ya kivuko cha MV Nyerere inatarajiwa kukamilika leo.

Idadi ya watu waliokufa kwenye ajali hiyo imeongezeka na kufikia 224 huku walio okolewa wakiwa hai ikiwa ni 41.