MASHIMO BARABARANI KUGHARIMU NAFASI ZA MABOSI TARURA

0
150

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa
amewataka watendaji wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kuacha utaratibu wa kuchimba barabara na kuziacha na mashimo kwa muda mrefu bila kuyafukia.

Ametoa maelekezo hayo alipokuwa akizungumza katika hafla ya utiaji saini mkataba wa mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji ya Tanzania (TACTIC) iliyofanyika mkoani Dar es Salaam.

Kwa upande wa Mameneja wa TARURA amewataka kuhakikisha bajeti ya kufukia mashimo inakuwepo pale ambapo wanakwenda kuchimba mashimo katika barabara.

Ameonya kuwaondoa katika nafasi zao watendaji wa TARURA pamoja na Mameneja wa TARURA wa mikoa na wilaya pale ambapo mashimo hayo yataachwa wazi hadi wiki mbili bila kuchukuliwa hatua zozote.

Waziri Mchengerwa amesema yapo mashimo yamechimbwa na kuachwa wazi mwezi mzima, hali inayosababisha adha kwa watumiaji wa barabara.