Marufuku kuingiza mifugo mapori ya Biharamulo, Buligi na Kimisi

0
1877

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amepiga marufuku wananchi kuingiza mifugo katika mapori ya akiba ya Biharamulo, Buligi na Kimisi.

Waziri Mkuu ambaye yuko ziarani mkoani Kagera amesema mapori hayo kwa sasa yapo katika hatua za mwisho kutangazwa kuwa mbuga za wanyama, hivyo kuifanya wilaya hiyo kuwa miongoni mwa wilaya za kitalii nchini.

Katika mkutano wa hadhara Biharamulo, Waziri Mkuu amemuagiza Meneja anayesimamia mapori hayo, Bigilamungu Kagoma kuhakikisha mapori hayo yanalindwa na hakuna mifugo inayoingizwa.

Amesema shilingi bilioni 70 zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji safi na salama katika wilaya ya Karagwe mkoani Kagera.