Manaibu Waziri Biteko na Mavunde wawacharukia wazalisha kokoto mkoani Dodoma

0
1547

Naibu Waziri wa Madini Dotto Biteko na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde Decemba 30 wametembelea kwa kushtukiza katika migodi ya machimbo ya kokoto katika eneo la Chigongwe Jiji la Dodoma ili kujionea shughuli za uchimbaji na usagaji mawe.

Ziara hiyo ni kutokana na agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa la kutaka wazalishaji wa kokoto waliopata tenda ya kusambaza kokoto katika ujenzi wa mji wa serikali kuongeza kasi ya uzalishaji ili iendane sambamba na kasi ya ujenzi ambapo mahitaji ya kokoto yamekuwa makubwa sana.

Naibu Waziri Biteko amezitaka Kampuni za Adili S.Y Dhiyeb na Loray Aggregates Company Ltd kuanza uzalishaji mara moja ifikapo tarehe 3.01.2019 ili kukidhi mahitaji ya kokoto katika ujenzi wa Mji wa Serikali na na kuwapa tahadhari ya kuwa ya kwamba ikidhihirika hawana uwezo huo wa kuendana na kasi ya ujenzi wa mji wa serikali,Wizara itapanua fursa hii ya usambazaji wa kokoto kwa wazalishaji nje ya mkoa wa Dodoma ili shughuli za ujenzi zisikwame.

Kwa upande wake naibu Waziri Mavunde ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini amewataka wazalishaji wa kokoto Dodoma kuitendea haki fursa hii waliyoipata ya uhakika wa soko la kokoto kupitia sekta ya ujenzi ambapo shughuli za ujenzi zimechukua kasi kubwa kwa kuhakikisha kwamba wanazalisha kwa wingi na kwa wakati muafaka.