Mamlaka ya viwanja vya ndege waendelea na ukarabati wa vyumba vya abiria

0
1143

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini Richard Mayongela amesema mamlaka yake imeanza kufanya marekebisho ya vyumba vya abiria katika viwanja vikubwa hapa nchini ili kuendana na mahitaji ya ongezeko la abiria kutokana na ujio wa ndege mpya za shirika la ndege Tanzania.

Mayongela amesema hayo katika Kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na Tbc, na kubainisha kuwa marekebisho katika viwanja vya ndege yanaenda sambamba na upanuaji wa viwanja kikiwemo kile cha Iringa.

Kuhusu mapato yatokanayo na viwanja vya ndege, Mayongela amesema katika kipindi cha miaka mitatu wameongeza zaidi ya Asilimia ishirinI ya mapato kutokana na kuboresha hudma na kupungza matumizi yasiyo na lazima kwa Asilimi kumi.

Pia amesema Jengo la Tatu la abiria na miundombinu yake katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere litakabidhiwa rasmi Mei mwaka huu ambapo litakuwa na uwezo wa kupokea abiria Milioni sita kwa mwaka.