Mamlaka ya bima kuchukua hatua kwa wanaogushi bima

0
1243

Mamlaka ya Usimamizi wa shughuli za bima nchini – TIRA imesema itaendelea kuwachukulia hatua za kisheria watakaobainika kughushi bima kutokana na baadhi ya watu wasio waaminifu kufanya vitendo hivyo.

Meneja wa Mamlaka hiyo Kanda ya Kati Stela Rutaguza ametoa onyo hilo jijini Dodoma kwenye semina ya kuwapatia elimu ya bima madiwani wa jiji hilo na kubainisha kuwa hivi sasa inawashikilia watu wanne kwa kosa la kughushi bima.

Baadhi ya madiwani walioshiriki semina hiyo wameomba elimu zaidi kuhusu bima kuendelea kutolewa kwa wananchi wa vijijini ili wajiunge na bima.