Malipo ya korosho kuanza kesho baada ya uhakiki

0
1603

Serikali imesema itaanza malipo ya wakulima wa zao la korosho kuanzia kesho Novemba 14 baada ya kukamilika kwa zoezi la uhakiki wa wakulima walio kusanya korosho zao katika vyama vya ushirika vya msingi.

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga amesema hayo mkoani Mtwara alipokuwa akizungumza na wadau wa zao hilo na kusema serikali inataka kuanza malipo ya wakulima hao kesho endapo watakamilisha zoezi la uhakiki wa wakulima waliokusanya korosho zao katika vyama hivyo.

 Waziri Hasunga, Naibu Waziri wa Kilimo Inocent Bashungwa na uongozi mzima wa wizara hiyo umewasili mkoani Mtwara lengo ikiwa ni kuhakiki kiasi cha korosho kilichokusanywa katika vyama vikuu mkoani humo.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amewatoa hofu wadau ambao wananufaika na biashara ya zao hilo.