Makamu wa Rais akutana na viongozi mbalimbali

0
2211

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) nchini Dkt Alex Mubiru ambaye alifika ofisini kwa Makamu wa Rais kujitambulisha.

Wakati wa mazungumzo yao, Makamu wa Rais amesema kuwa AfDB imeahidi kuendelea kushirikiana na kuisaidia Tanzania kutokana na hatua kubwa ya kimaendeleo ambayo imeonyesha.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi huyo wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Dkt Alex Mubiru amesema kuwa wawakilishi wa AfDB wapo nchini kwa lengo la kuisaidia serikali pamoja na watu wake.

Wakati huo huo Makamu wa Rais amekutana na kufanya mazungumzo na balozi wa Kenya nchini Dan Kazungu ambaye alifika ofisini kwa kwake kwa lengo la kujitambulisha.
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan pia amekutana na balozi wa Japan nchini Masaharu Yoshida ambaye amemaliza muda wake nchini.

Katika mazungumzo yao, Makamu wa Rais amemshukuru balozi Yoshida kwa ushirikiano wote alioutoa kwa kipindi chote alichokuwa hapa nchini.

Naye Balozi Yoshida ameishukuru serikali pamoja na raia wote wa Tanzania kwa ushirikiano mzuri waliompa kwa kipindi chake alichohudumu kama balozi wa Japan hapa nchini.