Makamu wa Rais aanza ziara Kigoma

0
2288

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ameanza ziara ya kikazi ya siku Nne mkoani Kigoma.

Katika siku yake ya kwanza ya ziara hiyo, Makamu wa Rais amepokea taarifa ya maendeleo ya mkoa wa Kigoma iliyosomwa na Mkuu wa mkoa huo Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga .

Akiwa mkoani Kigoma pamoja na mambo mengine, Makamu wa Rais atatembelea na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ile ya afya, elimu na mazingira.

Jumapili Septemba Tisa, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan atashiriki sherehe za kuwekwa wakfu Askofu Mkuu Msaidizi na Maskofu Wanne wa majimbo katika Kanisa la Pentekoste Mwanga lililopo katika Manispaa ya Kigoma – Ujiji.