Mahakamani kwa kuisabababishia serikali hasara ya mabilioni

0
1875

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita, Carlos Gwamagobe na watendaji watano wa halmashauri hiyo wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Geita kwa tuhuma za kughushi nyaraka,utakatishaji fedha na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya shilingi bilioni mbili nukta nane.

Watendaji hao wamesomewa mashtaka matano mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Geita Jovita Kato.

Kutokana na kosa la nne la  utakatishaji fedha kuwanyima dhamana watuhumiwa hao wamerudishwa rumande baada ya kesi yao kuahirishwa hadi tarehe 22 ya mwezi huu.

Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya makosa hayo kati ya mwezi  Januari  mwaka 2016 hadi mwezi Juni  mwaka huu.