Mahakama kuu kutoa uamuzi dhidi ya shauri la muswaada wa sheria

0
1054

Mahakama Kuu ya Tanzania Januari 14 inatarajia kutoa maamuzi dhidi ya shauri lililofunguliwa na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe na wenzie ya kupinga muswada wa mabadiliko ya sheria ya vyama vya siasa kujadiliwa bungeni

Mahakama hiyo imesikiliza pingamizi la Serikali dhidi ya shauri  la muswada wa Sheria ya marekebisho ya vyama vya Siasa wa mwaka 2018 chini ya Jaji Benhajji Masoud.

Pingamizi la serikali liliwasilishwa na Jopo la  mawakili wa serikali wakiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu Mark Mulwambo ambaye amedai kuwa Mahakama Kuu ya Tanzania haina mamlaka ya kusikiliza shauri la kupinga muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Vyama vya Siasa.


Kwa upande  wa walalamikaji wamedai kuwa Katiba inaipa mamlaka mahakama ya kusikiliza shauri hilo kwa sababu inatoa nafasi kwa mtu yeyote kupekea kesi pindi anapoona haki yake au katiba inavunjwa .