Magari yaonja Fly over Tazara

0
2416

Magari yameanza kupita katika daraja la juu – Fly over eneo la TAZARA wilayani Ilala katika jiji la Dar Es Salaam.

Wakazi wa jiji hilo waliopata fursa ya kutumia barabara hiyo wameelezea furaha yao wakipongeza jitihada za serikali kuboresha miundombinu hapa nchini.

Wamesema kuanza kutumika kwa barabara hiyo ya juu kutapunguza foleni ya magari katika eneo hilo.

Barabara hiyo ya juu inatarajiwa kufunguliwa rasmi mwezi ujao.