Kuchauka arejea kwenye kiti

0
2188

Mgombea ubunge katika jimbo la Liwale mkoani Lindi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zuberi Kuchauka ametangazwa kuwa mshindi wa kiti hicho.

Kuchauka ameshinda baada ya kupata kura 34, 532 ambazo ni sawa na asilimia 84.81 ya kura zote zilizopigwa.

Akitangaza matokeo hayo, msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Liwale, -Luiza Mlelwa amempongeza Kuchauka kwa kuaminiwa na Wakazi wa jimbo hilo na hivyo kuamua kumchagua ili aendelee kuwatumikia.

Katika uchaguzi huo mdogo wa ubunge kwenye jimbo la Liwale mkoani Lindi waliojiandikisha kupiga kura ni 55, 777, waliojitokeza kupiga kura ni 40706 na kura halali zilikuwa 40, 301.