KKKT yatoa pongezi kwa serikali

0
3964

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) limeipongeza serikali kwa kutoa huduma za matibabu ya moyo na figo nchini na hivyo kuwawezesha Watanzania wengi kumudu gharama za matibabu ya magonjwa hayo ndani ya nchi.

Pongezi hizo zimetolewa mkoani Kilimanjaro na Mkuu wa KKKT Askofu Fredrick Shoo wakati
wa mkutano mkuu wa 35 wa kanisa hilo.

Askofu Shoo ameiomba serikali kuongeza idadi ya madaktari pamoja na vitendea kazi ili kuwezesha Watanzania wengi zaidi kupatiwa matibabu hayo ya moyo na figo.

Akifungua mkutano huo, Mkuu huyo wa KKKT pia ameiomba serikali kuangalia namna ya kuondoa kodi ya ardhi kwa taasisi za kidini.

Akitoa salamu za serikali wakati wa mkutano huo mkuu wa 35 wa KKKT, Kaimu mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro – Kippi Warioba amesema kuwa serikali itaendelea kushirikiana na kanisa hilo katika kuwaletea maendeleo Watanzania.