Kivuko cha MV Nyerere chainuliwa kwa asilimia 85

0
2459

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo amesema zoezi la kukinasua kivuko cha MV Nyerere amesema vikosi vya ulinzi vimefanikiwa kukiinua kivuko hicho kwa asilimia 85 na kazi iliyobaki ni kutoa maji yaliyoingia kwenye kivuko.

Jenerali Mabeyo amesema wataalam wataendelea na kazi ya kutoa maji katika kivuko hicho na kukiweka pembeni kwa ajili ya ukaguzi.

Amevishukuru vyombo vya ulinzi na usalama kwa jinsi vinavyoendelea kuwezesha zoezi hilo huku akilipongeza Shirika la Utangazaji Tanzania –TBC kwa kuhabarisha umma yale yaliyokuwa yakiendelea baada ya kutokea kwa ajali hiyo.