Kilele cha Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar kinatarajia kifikiwa hapo Kesho ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapanduzi Dokta Ali Mohamed shein ndiye atakayekuwa mgeni rasmi.
Akizungumza na Tbc Kisiwani Pemba Waziri Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed amesema shughuli hizo zinatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri Aboud ametoa wito kwa wananchi kiziwani humo kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa Gombani ili kusherekea sherehe hizo.
Kauli mbiu ya maadhimisha ya Miaka 55 ya Mapindizi ni “’Mapinduzi yetu ndio Umoja wetu, Tuyalinde kwa maendeleo yetu”.