Kesi kupinga muswada wa vyama vya siasa bungeni yafutwa

0
1033

Mahakama Kuu ya Tanzania imeifuta kesi iliyofunguliwa na baadhi ya wabunge wa upinzani wakiongozwa na Zitto Kabwe ya kutaka kuzuia muswada wa kurekebisha vyama vya siasa usijadiliwe bungeni.

Hukumu hiyo imetolewa jijini Dar Es Salaam na Jaji Benhajo Masoud wa Mahakama Kuu nchini na kusema kesi hiyo imeonekana kuwa na dosari kutokana na kukiukwa kwa vifungu vya sheria.

Kesi hiyo ilikuwa ikipinga mjadala wa muswada wa kurekebisha vyama vya siasa katika bunge lijalo waliodai kuwa muswada huo unakiuka katiba na kukandamiza demokrasia nchini.

Pamoja na kuifuta kesi hiyo mahakama hiyo imewataka washtakiwa kuilipa serikali gharama za kuendesha kesi hiyo.

Hivyo kwa sasa baada ya kufutwa kwa kesi hiyo inamaanisha kuwa muswada huo sasa utajadiliwa bungeni kama ilivyopangwa.