Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango aitembelea TBC

0
2055

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dotto James ametembelea Shirika la Utangazaji Tanzania -TBC jijini Dar Es Salaam na kusema serikali inatambua changamoto zinazoikabili TBC na kuahidi kuzifanyia kazi.

Akizungumza na wafanyakazi wa TBC, Dotto amewapongeza wafanyakazi wa shirika hilo kwa kufanya kazi kwa ustahimilivu na kuahidi kutatua changamoto zinazoikabili TBC ili ifanye kazi kwa ufanisi.

 Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dkt. Ayub Rioba ameshukuru kwa ujio wa Katibu Mkuu James na kusema Shirika la Utangazaji Tanzania litaendelea kuwatumikia watanzania wote.

Hii ni ziara ya kwanza kwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango kutembelea TBC.