KATIBU MKUU FUATILIA MTANDAO WA WEZI FEDHA ZA MIRADI

0
152

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa amemuagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo kufuatilia mtandao wa wizi wa fedha za miradi.

Mchengerwa ametoa agizo hilo wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji ya Tanzania (TACTICS) iliyofanyika mkoani Dar es Salaam.

Amesema eneo la fedha za miradi lina changamoto, hivyo amemtaka Katibu Mkuu TAMISEMI kufuatilia mtandao huo wa wizi ili kubaini watumishi wa TAMISEMI wanaohusika.

Kwa mujibu wa Waziri Mchengerwa, kwa
sasa ana ushahidi wa halmashauri tano ambazo baadhi ya viongozi wa halmashauri hizo na Watumishi wanadaiwa kugawana fedha za miradi.