Kampuni ya uchimbaji madini yapigwa stop

0
1378

Naibu Waziri wa Madini Dotto Biteko ameiagiza kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya MMC inayofanya kazi katika kijiji cha Mangae na Mtipule wilayani Mvomero mkoani Morogoro kusimamisha uzalishaji hadi hapo watakapokamilisha taratibu za kisheria za madini.

Akikagua kazi zinazofanyika katika mgodi huo Naibu Waziri Biteko amesema kampuni hiyo inapaswa kuwalipa fidia wananchi walioondolewa katika eneo hilo.

Halikadhalika amewaonya baadhi ya watanzania wanaoingia mikataba na wawekezaji kutoka nje ambao hawafuati taratibu za nchi.

Mkuu wa wilaya ya Mvomero Mohamed Utali ameahidi kusimamia utekelezaji wa ulipwaji fidia wananchi huku mwakilishi wa kampuni ya MMC Daniel Augustino akisema watazifanyia kazi changamoto zilizojitokeza.