Kamati za mitihani zatakiwa kufanya kazi kwa uadilifu

0
2260

Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) limeziagiza kamati za mitihani za mikoa na halmashauri zote nchini kuhakikisha taratibu zote za uendeshaji wa mitihani ya taifa ya darasa la saba zinazingatiwa.

Agizo hilo limetolewa jijini Dar es salaam na Katibu Mtendaji wa NECTA Dkt Charles Msonde na kuhimiza mazingira yote ya vituo vya kufanyia mitihani kuwa salama na kuzuia aina yoyote ya udanganyifu.

Dkt Msonde pia amewataka wamiliki wa shule kutoingilia majukumu ya wasimamizi wa mitihani katika kipindi chote cha mitihani.

Mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi utafanyika Septemba Tano na Sita mwaka huu ambapo watahiniwa waliosajiliwa ni zaidi ya Laki Tisa na Sitini Elfu katika shule 16,845.