JITIHADA ZA TANZANIA KUBORESHA MIFUMO YA CHAKULA

0
153

Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango ametaja namna Tanzania imedhamiria kufikia lengo namba mbili la umoja wa mataifa (SDG2) linalohusu kuufikia ulimwengu usio na njaa mwaka 2030.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa Mifumo ya Chakula Afrika unaofanyika mkoani Dar es Salaam Dkt. Mpango amesema mkutano huo utainufaisha Tanzania kuimarifa mifumo ya chakula kwa kuwekeza zaidi kwenye rasilimali ardhi na nguvu kazi ya Wanawake barani Afrika.

Amesema Tanzania inajivunia jitihada za maboresho ya mifumo ya chakula na imejitoa kushirikiana na wengine ambapo lengo kuu ni kuwa na ulimwengu usio na njaa ifikapo mwaka 2030.

Akitoa mifano ya namna Tanzania imeweka jitihada kwenye suala hilo Dkt. Mpango amesema, hivi sasa kilimo hapa nchini kinatambulika kama chanzo kikuu cha ukuaji wa uchumi ambapo kimetoa ajira kwa zaidi ya asilimia 65 ya Wananchi huku kikichangia katika pato la Taifa kwa asilimia 27 Tanzania Bara na asilimia 21 kwa Zanzibar.

Amesema sekta ya kilimo inachangia katika usafirishaji wa bidhaa zake nje ya nchi [export] kwa zaidi ya asilimia 30 na kuzalisha asilimia 65 za malighafi kwa ajili ya viwanda vya Tanzania.