Iddi Simba afariki dunia

0
406

Aliyewahi kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara katika Serikali ya awamu ya tatu, Iddi Simba amefariki dunia hii leo.

Taarifa zilizothibitishwa na mtoto wake Sauda Kilumanga zinaeleza kuwa, Iddi Simba amefariki dunia katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.