Idadi ya waliokufa kwenye kivuko yaongezeka

0
2642

Idadi ya watu waliokufa maji kufuatia kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere imeongezeka na kufikia zaidi ya mia moja.

Miili zaidi imepatikana kufuatia kazi ya uokoaji inayoendelea hivi sasa katika eneo kilipozama kivuko hicho.

Kivuko cha MV Nyerere kinachotoa huduma zake kati ya Bugorora na Ukara wilayani Ukerewe mkoani Mwanza kilizama Alhamisi Septemba 20 mwaka huu kikiwa katika safari zake za kawaida.

Rais John Magufuli ametuma salamu za pole kwa Watanzania wote kufuatia ajali hiyo na kuwataka kuwa watulivu katika kipindi hiki wakati shughuli za uokoaji zikiendelea.