Dkt Ndumbaro Naibu Waziri mpya Mambo ya Nje

0
2386

Rais John Magufuli amemteua Dkt Damas Ndumbaro kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Dkt Ndumbaro ambaye ni Mbunge wa Songea mjini mkoani Ruvuma anachukua nafasi ya Dkt Susan Kolimba ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Wakati huo huo Rais Magufuli amemteua Dkt Faraji Mnyepe kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Dkt Mnyepe anachukua nafasi ya Profesa Adolf Mkenda ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Profesa Mkenda amechukua nafasi ya Meja Jenerali Mstaafu Gaudence Milanzi ambaye amestaafu.

Uteuzi wa viongozi hao umeanza leo Septemba 26 na tarehe ya kuapishwa kwao itatangazwa baadaye.