Dkt Dalmas kuongoza bodi TANROADS

0
1978

Rais John Magufuli amemteua Dkt Dalmas Nyaoro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS).

Dkt Nyaoro ambaye ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam anachukua nafasi ya Hawa Mmanga ambaye amemaliza muda wake.

Uteuzi wa Dkt Nyaoro umeanza Oktoba Kumi mwaka huu.