Dkt. Biteko asisitiza upendo na umoja kwa Watanzania

0
155

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amewasisitiza wananchi kushikamana kuwa na umoja pamoja na upendo ili kuweza kuleta maendeleo ya pamoja kwenye jamii na kuacha kufanyiana chuki na kugawanyika kutokana na tofauti mbalimbali zikiwemo za itikadi za vyama, dini, kabila na majimbo.

Dkt. Biteko ameyasema hayo wakati akihutubia wananchi wa jimbo lake la Bukombe mkoani Geita katika ziara yake mkoani humo.

“Nataka niwaombe tupendane, tuthaminiane. Tofauti tulizonazo zisitufanye tukagawanyika, tuonane sisi ni  Watanzania wa daraja moja. Niwaombe viongozi wa chama cha CCM na madiwani mliopo hapa twendeni tukawaunganishe Watanzania,” amesema Dkt. Biteko

Dkt. Biteko amefanya ziara wilayani Bukombe mkoani Geita akitokea Geita Mjini alipofungua rasmi Maonesho ya Sita ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea mkoani humo mpaka Septemba 30, 2023 yatakapofungwa na Rais Samia Suluhu Hassan