CCM yashiriki mbio za kuchangia watoto wenye Saratani nchini

0
137

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo ameshiriki mbio za Kilomita 5 zilizoandaliwa na Benki ya CRDB kwa lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya kugharamia matibabu kwa watoto wenye Saratani na utunzaji wa mazingira nchini.

Mbio hizo zimeanzia katika viwanja vya Green Park Osterbay ambapo Mgeni Rasmi alikua Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa.

CCM imeshiriki mbio hizo kwa lengo la kusambaza tabasam kwa watoto wenye Saratani na pia kushiriki katika utunzaji wa mazingira