CCM yaibuka kidedea katika majimbo ya Monduli na Ukonga

0
2100

Msimamizi wa uchaguzi katika jimbo la Ukonga jijini Dar es salaam Jumanne Shauri amemtangaza mgombea wa ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mwita Waitara kuwa mshindi katika kinyang’anyiro hicho.

Waitara ameshinda baada ya kupata kura 77,795 ambazo ni sawa na asilimia 89.19.
Uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo hilo la Ukonga na jimbo la Monduli mkoani Arusha ulifanyika septemba 16 mwaka huu.

Katika jimbo la Monduli, CCM imeibuka kidedea katika uchaguzi huo mdogo ambapo mgombea wake Julius Kalanga ameshinda kwa asilimia 95.

Akitangaza matokeo hayo, msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo la Monduli, – Steven Ulaya amesema kuwa Kalanga ameshinda kwa kupata kura 65, 714.