Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Mussa Assad tayari amewasili katika ofisi za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huko jijini Dodoma ili kuhojiwa na Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge.
Profesa Assad ameitikia wito wa Spika wa Bunge Job Ndugai aliyemtaka afike mbele ya kamati hiyo kufuatia kauli yake aliyoitoa kwa Bunge kuwa ni dhaifu.
Katika ofisi hizo za Bunge jijini Dodoma, Profesa Assad amepokelewa na Mwenyekiti wa kamati hiyo ya Bunge ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge, – Emmanuel Mwakasaka.