Bodi mpya ya NECTA yazinduliwa

0
2329

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako ameiagiza bodi mpya ya Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kusimamia utungaji na uendeshaji wa mitihani kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa katika kuboresha kiwango cha elimu nchini.

Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo jijini Dar es salaam wakati wa kuzindua bodi hiyo mpya ya Baraza la Mitihani la Taifa na kuongeza kuwa uteuzi wa bodi hiyo mpya utaleta tija katika usimamizi na udhibiti ubora wa elimu nchini.

Katika kuboresha udhibiti wa udanganyifu wa mitihani nchini, Waziri Ndalichako amesema kuwa serikali imenunua mashine itakayofunga mitihani yenyewe huku akiwaonya walimu watakaojihusisha na wizi wa mitihani kuwa serikali haitawavumilia.

Bodi hiyo mpya ya Baraza la Mitihani la Taifa iliyozinduliwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako inajumuisha wajumbe Tisa ambao watafanya kazi kwa miaka mine.