Bilioni Moja atakayefanikisha kupatikana kwa MO

0
2169

Familia ya mfanyabiashara maarufu nchini Mohamed Dewji maarufu kama MO ambaye alitekwa siku chache zilizopita na watu ambao hawajafahamika hadi hivi sasa jijini Dae es salaam imetangaza zawadi ya Shilingi Bilioni Moja kwa mtu yoyote atakayefanikisha kupatikana kwa mfanyabiashara huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, mmoja wa wanafamilia wa mfanyabiashara huyo Azim Dewji amesema kuwa taarifa za mtu atakayefanikisha kupatikana kwa MO zitakua siri.

Azim amesema kuwa mtu yeyote mwenye taarifa hizo awasiliane na familia kupitia namba 0755 030014 na 0717 208478.

Familia ya Dewji pia imeishukuru serikali pamoja na vyombo vyote vya ulinzi na usalama kwa jitihada kubwa walizofanya kuhakikisha kuwa MO anapatikana akiwa salama.

Pia imewashukuru Watanzania wote kwa maombi  na dua zao.