Baraza Wawakilishi kukutana Septemba 19

0
2037

Mkutano wa 11 wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar unatarajiwa kuanza Septemba 19 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Unguja, Katibu wa Baraza la Wawakilishi Raya Issa Msellem amesema kuwa wakati wa mkutano huo maswali 154 yataulizwa na kujibiwa.

Ameongeza kuwa miswada mitatu ya Sheria itawasilishwa katika Baraza hilo la Wawakilishi Zanzibar na kusomwa kwa mara ya kwanza.