Bajeti ya wizara ya Ulinzi yapita

0
306

Bunge limepitisha bajeti ya wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 ambapo wizara hiyo imeomba kupatiwa zaidi ya shilingi trilioni 2.7 kwa ajili ya matumizi ya kawaida na shughuli za maendeleo.

Bajeti hiyo iliwasilishwa bungeni jijini Dodoma na.waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Stergomena Lawrence Tax, ambapo Wabunge kadhaa walipata fursa ya kutoa michango yao.