Ajali yaua watano Bukoba

0
448

Watu watano wamefariki duniani na wengine tisa kujeruhiwa baada ya gari lenye namba za usajili T471DCG kufeli breki na kuingia mtaroni eneo la round-about ya Rwamishenye, Manisapaa ya Bukoba.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera, Revocatus Malimi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.