Waziri wa Ulinzi wa Marekani aachia ngazi

0
1213
Mandatory Credit: Photo by Sonu Mehta/Hindustan Times/REX/Shutterstock (9870611d) Defence Secretary of US James Mattis speaks during the joint statement in which Secretary of State Mike Pompeo, Union External Affairs Minister Sushma Swaraj and Defence minister Nirmala Sitharaman were also present, at Ministry of External Affairs in Jawaharlal Nehru Bhawan in New Delhi, India. US Defense Secretary James Mattis and Secretary of State Mike Pompeo visit to India - 06 Sep 2018 The United States and India signed the high-level COMCASA defence agreement today that will allow India to buy advanced American military hardware.

Waziri wa Ulinzi wa Marekani James Mattis leo ametangaza kujiuzulu wadhifa wake.

Katika barua yake ya kujiuzulu, Mattis amesema anaamini kwamba Marekani inahitaji kuendeleza ushirikiano imara na washirika wake, na inapaswa kuweka msimamo usio na utata dhidi ya mataifa ya China na Russia.

Mattis ambaye ni mwanajeshi aliyestaafu akiwa na cheo cha Jenerali, amekuwa akichukuliwa kama mhimili wa utulivu katika baraza la mawaziri la Rais Donald Trump wa Marekani.

Uamuzi huo wa Mattis umekuja baada ya tangazo la Rais Trump la kuondoa wanajeshi wa Marekani nchini Syria, hatua ambayo imewakasirisha washauri wake na washirika wa Marekani.

Hata hivyo Rais Trump wa Marekani amesema atatangaza mrithi wa Mattis hapo baadae.