Waliokufa Afghanistan wafikia 68

0
2122

Idadi ya watu waliokufa baaada ya kutokea kwa shambulio la kujitoa muhanga nchini Afghanistan imeongezeka na kufikia 68.

Polisi nchini Afghanistan  wamesema kuwa shambulio hilo ambalo limetokea katika jimbo la Nangarhar lililopo karibu na Pakistan ni baya kuwahi kutokea katika miezi ya karibuni nchini humo.

Katika tukio hilo watu wengine 165 wamejeruhiwa.

Mpaka  sasa hakuna kikundi chochote kilichodai kuhusika na shambulio hilo la kujitoa muhanga, lakini inadhaniwa kuwa wanamgambo wa Kiislam ndio wametekeleza tukio hilo kwa kuwa wamekua wakifanya mashambulio mengi ya kujitoa muhanga katika jimbo hilo.

Mamia ya raia wa Afghanistan wameuawa katika mashambulio yaliyotokea kwenye kipindi hiki ambacho nchi hiyo inajiandaa kufanya uchaguzi wa Wabunge mwezi Oktoba mwaka huu.

Serikali ya Afghanistan  imeonya kuwa mashambulio mengi yatatokea katika mikutano mbalimbali ya kampeni, hivyo ni muhimu kwa raia wa nchi hiyo kuchukua tahadhari.