Wakimbizi wasubiri kuingia Marekani

0
1652

Wakimbizi kutoka nchi za Amerika ya Kati hasa Honduras walioko njiani kwenda Marekani kutafuta maisha mazuri wamesema kuwa, wana matumaini ya kupata ridhaa ya kuingia nchini humo licha ya vikwazo vingi.

Wakimbizi hao wamesema kuwa matumaini yao yote yako nchini Marekani, kwani katika nchi wanazotoka wamekatishwa tamaa na mambo mbalimbali wakiwa hawana njia nyingine ya kujikimu.

Mkimbizi mmoja mwanamke mwenye mtoto mdogo, yeye amebainisha kuwa alikuwa akilazimishwa kuuza dawa za kulevya katika baa ili aweze kujitafutia maisha, la sivyo maisha yake yangekuwa hatarini.

Ameongeza kuwa amekuwa akiishi maisha ya kubahatisha na kwamba hata kama zoezi la kuingia nchini Marekani litakuwa refu atasubiri.