Waamriwa kuondoka katika maeneo yao

0
1894

Zaidi ya watu Laki Tano wameamriwa kuondoka haraka katika makazi yao yaliyopo kwenye eneo la kusini mashariki  nchini Marekani ili kuepusha madhara yanayoweza kujiyokeza katika kipindi hiki ambacho kimbunga Michael kinakaribia kulikumba eneo hilo.

Watu hao ni wa majimbo ya Alabama, Florida na Georgia ambapo pia majimbo hayo yametangaza hali ya hatari.

Watabiri wa hali ya hewa nchini Marekani wamesema kuwa kimbunga hicho cha Michael kwa sasa kimekwishaingia katika hatua ya tatu na kuongeza kasi yake kadri kinavyopita kwenye ghuba ya Mexico kuelekea  majimbo ya Florida, Alabama na Georgia.

Wamesema kuwa kimbunga hicho ambacho ni hatari zaidi kinasababisha upepo mkali ambao unakwenda kwa kasi ya kilomita mia mbili kwa saa.