Uturuki na Marekani kuimarisha uhusiano

0
1830

Mkuu wa Shirika la Ujasusi la nchini  Uturuki, –  Hakan Fidan amekutana na kufanya mazungumzo na Wabunge wa  Bunge la Marekani pamoja na maafisa wa kijasusi wa nchi hiyo.

Lengo la mkutano huo ni kuimarisha uhusiano uliozorota mwaka 2017 baina ya Uturuki na Marekani, nchi ambazo ni wanachama wa Jumuiya ya Kujihami ya nchi za Magharibi (NATO).

Fidan ambaye ni mshirika wa karibu wa Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki  amekutana na Wabunge hao wa Bunge la Marekani na kujadili masuala yanayohusu NATO na pia alitarajiwa kukutana na maafisa wa kijasusi  wa nchi hiyo.

Mauaji ya mwandishi wa habari wa Saudi Arabia, – Jamal Khashoggi katika ubalozi mdogo wa nchi hiyo nchini Uturuki,  ni miongoni mwa masuala yaliyojadiliwa katika mkutano huo wa Mkuu wa Shirika la Ujasusi la nchini  Uturuki  na Wabunge wa  Bunge la Marekani pamoja na maafisa wa kijasusi wa nchi hiyo.

Wabunge wa Bunge la Marekani wanataka kuiadhibu Saudi Arabia kwa mauaji hayo ya Khashoggi, licha ya uamuzi wa Rais Donald Trump wa Marekani kuikingia kifua Saudia Arabia, nchi ambayo ni mshirika wake wa  muda mrefu.