Umoja wa Mataifa kuchunguza umaskini Uingereza

0
1605

Baadhi ya watu walionusurika kufa wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe nchini Ivory Coast, vita iliyosababisha Rais Laurent Gbagbo kuondoka madarakani, wanaitaka serikali ya nchi hiyo iwalipe fidia.

Watu hao wamefikisha shauri lao mahakamani na kusema kuwa wanatamani kuona wahusika na mauaji hayo pamoja na vitendo vingine vya ukatili wakati wa miaka saba ya vita hiyo wanachukuliwa hatua za kisheria.

Wamesema kuwa wanapatwa na hasira wanapowaona wahalifu wa vita hiyo wakiendelea kuishi kwa amani bila ya kuchukuliwa hatua yoyote.

Vita hiyo ilizuka kati ya askari waliokuwa wakimtii rais wa zamani wa nchi hiyo Laurent Gbagbo dhidi ya wafuasi wa Alassane Dramane Ouattara ambaye alitangazwa mshindi wa kiti cha Urais.

Takribani watu elfu tatu waliuawa wakati wa vita hiyo.