Ujumbe wa Afghanistan wawasili Pakistan kwa ajili ya mazungumzo

0
922

Ujumbe wa serikali ya Afghanistan umewasili nchini Pakistan ukijaribu kuishawishi serikali ya nchi hiyo kuwashawishi wapiganaji wa kikundi cha Taleban wa nchini Afghanistan kukubaliana na mpango wa amani wa nchi yao.

Kumekuwa na wapiganaji wa kikundi cha Taleban katika nchi za Pakistan na nchini Afghanistan, wote wakipigana dhidi ya serikali ya nchi zao.

Serikali ya Afghanistan kwa upande wake ilifanikiwa kufikia mkataba nawapiganaji wa Taleban nchini humo ili kurejesha amani.

Serikali ya Afghanistan imeiomba serikali ya Pakistan kuwashawishi wapiganaji wa Taleban wa Afghanistan kuitambua serikali ya nchi yao iliyoko madarakani na hatimaye pande hizo kuweza kukaa katika meza ya mazungumzo.