Uingereza,Ujerumani na Ufaransa zataka uchunguzi kuhusu Khashoggi

0
1967

Uingereza,Ujerumani na Ufaransa zimetaka kufanyika kwa uchunguzi wa kina kufuatia kutoweka kwa mwandishi maarufu wa wa habari wa Saudia Arabia, – Jamal Khashoggi.

Mawaziri wa mambo ya nje wa nchi hizo wamesema kuwa iwapo mtu yoyote atabainika kuhusika na kutoweka kwa mwandishi huyo awajibike.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, – Jeremy Hunt amesema kuwa mambo yote yanayoendelea hivi sasa yanaihusu Saudi Arabia licha ya nchi hiyo kukanusha kuhusika na kutoweka ama kuuawa kwa Khashoggi katika ubalozi wake huko Instanbul nchini Uturuki.

Khashoggi aliyekuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya Saudia Arabia alitoweka tangu Oktoba Pili mwaka huu baada ya kuingia katika ubalozi wa nchi hiyo mjini Instambuli nchini Uturuki.

Naye Rais Donald Trump wa Marekani amesema kuwa litakua ni jambo la kusikitisha endapo itabainika Saudi Arabia imehusika na kutoa maagizo ya kuuawa kwa Khashoggi