Ufaransa kutoongeza kodi ya mafuta

0
1526

Waziri Mkuu wa Ufaransa, – Edouard Philippe anatarajiwa kutangaza uamuzi wa serikali ya nchi hiyo wa kubatilisha mpango wake wa kuongeza kodi kwenye mafuta, ongezeko lililokua lianze Januari Mosi mwaka 2019.

Uamuzi huo wa serikali ya Ufaransa umelenga kutuliza ghasia pamoja na maandamano ya takribani wiki mbili  yanayofanywa na wanaharakati ili kupinga ongezeko hilo la kodi.

Ghasia na maandamano  hayo nchini Ufaransa yalianza mwezi Novemba mwaka huu baada ya serikali ya nchi hiyo kutangaza azma yake ya kuongeza kodi ya mafuta ikiwa ni sehemu ya jitihada za kupambana na mabadiliko ya Tabia Nchi.